Home  |  Shelly  |  The Calmes  |  Neema House Church  |  Manna  Care Center 
Help Us  |    Contact Links  |  TUFUNDISHE Kigazeti


TUFUNDISHE Kigazeti

Njia ya Kufundisha Maombi

 

MUNGU ANATAKA KUTUSIKILIZA SISI

LENGO: Kuwasaidia wanafunzi watambua umuhimu wa mawasiliano kati yetu sisi na Mungu Baba yetu.

Wasaidie wanafunzi wajue kuwa Mungu anataka sisi tuongee naye muda wowote na mahali popote, iwe nyumbani, katika gari, kanisani, shule, sokoni, nje au kiwanjani. Haijalishi muda gaani na sehemu gani.

Endelea kuwaelezea wanafunzi kuwa ingawa Mungu hatumwoni kwa macho yeye bado yupo pamoja nasi na anataka sisi tuongee naye popote tunapokuwa. Nafikiri tusijisikie vibaya au kujihisi wapweke kama uko na mtu halafu yeye anakuwa hakujali anakuwa kama ana shughuli zake tu.

Toa mfano huu: Wanafunzi wawili wawili watoke mbele kundi mojamoja. Kisha katika hilo kundi la wanafunzi wawili mmoja azungumze na mwenzie. Na huyo mwenzie awe hata hamsikilizi wala kumjali huyu anayeongea naye. Aangalie pembeni tu na kufanya shughuli zake. Kisha muulize yule aliyekuwa akiongea anajisikiaje? Pengine atasema alijisikia kukataliwa na hata hasira kidogo pengine.

Waambie wanafunzi kuwa vivyo hivyo Mungu naye hujisikia kukataliwa na kusahauliwa pale tunapokuwa hatuongei naye au kutambua uwepo wake. Anaweza hata asijisikie hasira bali atajisikia kukosa ushirikiano na sisi.

Wakumbushe kuwa Mungu daima hatuachi sisi wapweke. Yupo nasi muda wote. Kila siku Yeye yupo tayari kusikiliza matatizo yetu, mahitaji yetu na shukurani zetu. Anataka kushirikiana na sisi katika kila kitu tunachokifanya na kutusaidia kwa njia yoyote awezayo. Na tunaweza kuongea na Mungu kwa njia ya maombi tu.

TUFUNDISHE April/May 2008 Vol. 1 No. 6

Back to index

 
Animated flag by
 
www.3DFlags.com
Web Editor - Don Tarvin
Updated 26 Sep 2008