Home  |  Shelly  |  Let's Hope:  Helping Others with Purpose and Essentials
Swahili Kids Ministries  |  Help Us  |  Contact Links  |  TUFUNDISHE Kigazeti


TUFUNDISHE Kigazeti

Neno la Mungu Kuhusu Uinjilisti Wa Watoto

 

KUWASADIA WATOTO KUKUA KIROHO

Itakuwa ni ajabu na kitu cha kushangaza sana iwapo mtoto ataweza kutambua mahitaji yake ya chakula cha kiroho kama anavyohitaji chakula cha kawaida kama nyama. Watoto wanahitaji kujua jinsi ya kutii amri iliyopo katika 2 Petro 3:18, “Lakini kueni katika neema na katika kumjua Bwana wetu na mwokozi Yesu Kristo”. Pia watoto wanahitaji kutiwa moyo na kutambua maendeleo yao ya kiroho.

Wafundishe watoto katika njia hizi nne na uwe tayari kuwasaidia.

1. KWENDA KANISANI KWENYE DARASA LA WATOTO
Wahimize watoto wampe Mungu muda waeleze umuhimu alioutoa Mungu katika kukusanyika pamoja kumwabudu. Waebrania 10:25, “Wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.”

Wafundishe kuwa makini katika kusikiliza Neno. Watie moyo kuuliza na kujibu maswali ya udadisi kama: Nani? Nini? Lini? Wapi? Kwa nini?

Mfano wa Maswali:
* “Somo la leo linafundisha kuhusu nani?”
* “Nini kilitokea katika somo la leo?”
* “Je, ilitokea lini?”
* “Je, somo hili inapatikana wapi kwenye Biblia?”
* “Je, ni kwa nini somo hili ni muhimu kwangu?”

Kama ukiuliza mara kwa mara maswali haya, basi utakuwa umejenga maswali haya akilini mwao. Mwishowe wataanza kujiuliza maswali haya wenyewe na kujikuta wameanza kujilisha chakula cha kiroho wenyewe kanisani.

2. KUSOMA NENO LA MUNGU NA KUOMBA
Wasaidie watoto waweke kipindi cha peke yako na Mungu kwenye ratiba zao za kila siku. Ingawa watoto wa siku hizi wanajali sana na kutambua umuhimu wa muda kwa kupitia kutiwa moyo na kuhimizwa wanaweza kutenga hata dakika 10 au 15 kusoma Neno, kujikumbusha mistari ya Biblia na kuomba.

Je, wanapaswa kusoma nini?
Tumia kitabu cha masomo ya watoto pamoja na Biblia ya watoto. Anzisha usomaji wa Biblia ya watoto nzima katika njia rahisi na inayoweza kueleweka wasome mistari michache kwa kila siku. Ili waweze kujilisha Neno la Mungu wanaposoma wanapaswa kujiuliza maswali haya.

“Je, mstari huu au maneno haya yanasemaje?”
“Je, maana yake ni nini?”
“Je, Mungu ananiambia nini hapa?”

Kama watapata nafasi ya kuandika majibu kwenye daftari itakuwa ni rahisi kuwa kujifunza kwa undani kuhusu mistari hiyo ambayo Mungu anasema.
Soma Timotheo 4:13

Je, wanapaswa kujikumbusha nini?
Ni vizuri kama watajikumbusha mstari waliopewa na mwalimu kujifunza na mstari ambao umewagusa na kuongea na mioyo yao; pia mistari ambayo inafahamika na wengi kama vile Zaburi 1 au Zaburi 23.

Je, mtoto ale kwa muda gani kila siku? Kama jinsi chakula cha mwili kinavyowatia nguvu watoto, ndivyo jinsi ulaji wa mara kwa mara wa Chakula cha Kiroho unavyowajenga na kuwatia nguvu kiroho.

3. KUMTII MUNGU SIKU KWA SIKU
Soma kwa makini 1 Yohana 2:3. Na katika hili twajua ya kuwa tunamjua yeye ikiwa tunazishika amri zake. Pia mtoto hupata Chakula cha Kiroho hata anaposikiliza sauti ya Mungu.

Mchezaji mmoja alipokuwa katika dakika za mwisho za mchezo timu yake ilifungwa goli lingine la ushindi lakini, badala ya kukasirika na kuchukia, alimwambia Mungu amtie nguvu ili awe mchezaji mwema. Huyu alimtii Mungu na kumtegemea.

Mtoto wa Mungu lazima awe tofauti popote anapotembea. Hebu waulize watoto swali hili, “Je, Mungu alikusudia vipi ili umtii yeye katika wiki iliyopita?” Wachukue nafasi ya kumsifu Mungu kwa jinsi alivyofanya kazi kwa watoto ili wafanye mapenzi yake. Soma Wafilipi 2:13.

4. KUTOA USHUHUDA
Mtoto hupenda kuwashirikisha wenzie juu ya imani yake. Mtu anayetoa ushuhuda ni yule anayetoa ushahidi. Hivyo basi, watie moyo watoto kutoa ushuhuda siyo tu juu ya wokovu, bali pia jinsi Mungu anavyofanya kazi ndani yao.

Mtoto anaweza kuwaeleza wenzake jinsi Mungu alivyojibu maombi yake, jinsi alivyojifunza kutoka kwenye Neno la Mungu, jinsi Mungu alivyompa ujasiri wa kuwapongeza wachezaji wa timu nyingine ingawa timu yake ilishindwa, na jinsi Mungu alivyomsaidia asiende kuangalia video mbaya.

Kama mtoto mmoja ataweza kutoa ushuhuda na jinsi Mungu alivyofanya kazi ndani yake, watoto wengine watatiwa moyo kusimama imara pia. Ikiwa watajengewa msingi wa nidhamu hii ya maisha ya kikristo, basi wataendelea kukua hata wakiwa peke yao.

Ni wajibu wetu kuwafundisha watoto jinsi vile Mungu anavyofanya kazi kwenye maisha ya watu wengine, ili waweze kujifunza na kuona kweli Mungu anaweza kubadilisha maisha ya watu na inawezekana kabisa kuishi maisha ya kumpendeza Mungu. Pia, tuwatie moyo katika maisha yao ya kiroho kila siku ili waweze kusonga mbele katika maisha yao ya kila siku.

TUFUNDISHE April/May 2008 Vol. 1 No. 6

Back to index

 
Animated flag by
 
www.3DFlags.com
Web Editor - Don Tarvin
Updated 16 Aug 2011