Home  |  Shelly  |  The Calmes  |  Neema House Church  |  Manna  Care Center 
Help Us  |    Contact Links  |  TUFUNDISHE Kigazeti


TUFUNDISHE Kigazeti

Maswali Magumu Yaulizwayo na Watu WENGI

 


Je, Mungu bado anaendelea kufufua wafu hadi siku hizi?

Katika kipindi cha Biblia Mungu mara nyingine alifufua watu waliokufa wakawa na afya tena. Na alitumia watu wake maalumu kufanya muujiza huu wa aina yake. Soma Wafalme 17:24, Luka 7:16, Yohana 11:42-45 na Matendo 9:40-42.

Aliwatumia manabii (Elisha na Elia). Alitumia mtoto wake (Yesu) pekee. Aliwatumia mitume (Petro na Paulo) pia. Watu hawa walihakikisha katika namna ya kushangaza sana kuwa maneno yao yalitoka kwa Mungu. Hivyo maneno hayo (na maneno ya wengine Mungu aliowachagua) yaliandikwa kisha baadae yakaunganishwa na kuitwa ‘Biblia’.

Mungu bado ana uwezo wa kuwafufua watu kutoka katika wafu na tayari ameshatuonyesha sisi uwezo wake huo katika Biblia. Hivyo tunaweza kuamini tu kwamba uwezo huo anao. Sio lazima hadi tuone mtu amemfufua mtu aliyekufa. Hili ndiyo tuamini kuwa Mungu anaweza. Watu wakikataa kuliamini Neno la Mungu hata wakimuona mtu anafufuka toka kwa wafu haitoshi kuwashawishi kuwa ni kweli. Soma Luka 16:31.

Mungu ataendelea kuwa na uwezo huo wa kufufua wafu hata kama alifanya siku hizo au hata asipofanya. Yesu atakaporudi mara ya pili atamfufua kila Mkristo. Ila hautakuwa na mwili wako huu uliouzoea kama wa Lazaro aliyefufuliwa na Yesu au wa wale wengine waliofufuliwa. Tunasoma habari zao katika Biblia.

Utapata mwili mpya kama ule Yesu aliokuwa nao ule ambao hautakufa tena bali utaishi milele. Soma 1 Wakorintho 15:35-58 na 1 Wathesalonike 4:26.

Back to index

TUFUNDISHE April/May 2008 Vol. 1 No. 6

 
Animated flag by
 
www.3DFlags.com
Web Editor - Don Tarvin
Updated 26 Sep 2008